Chanzo cha picha, IDF
Jeshi la Israel limesema limeupata na kuutambua mwili wa kiongozi wa Hamas Mohammed Sinwar, wiki tatu baada ya Israel kutangaza wamemuua katika shambulizi la angani.
Mwili wake uligunduliwa kwenye handaki chini ya Hospitali moja katika mji wa kusini wa Khan Younis, Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) lilisema Jumapili.
Taarifa kutoka Jeshi hilo imesema uchunguzi wa chembechembe za vinasaba DNA vimethibitisha kuwa ni mwili wa Sinwar - ingawa Hamas haijathibitisha hadharani kifo chake.
Sinwar, 49, aliuawa katika shambulizi la anga la Mei 13, ambalo shirika la ulinzi wa raia linaloendeshwa na Hamas lilisema liliua watu 28 na kujeruhi kadhaa.
Mwili wa Sinwar ulipatikana pamoja na ule wa Mohammad Sabaneh, kamanda wa Kikosi cha Hamas cha Rafah, IDF ilisema.
Iliongeza kuwa "vitu kadhaa vya Sinwar na Sabaneh vilipatikana, pamoja na matokeo ya ziada ya kijasusi ambayo yalikusanywa kwa uchunguzi zaidi".
IDF ilisema miili mingine ilipatikana, ambayo ilikuwa ikiendelea kuitambua.
Soma zaidi