Mashambulizi makubwa zaidi ya ndege zisizo na rubani yatokea Ukraine

15 hours ago 8

.

Chanzo cha picha, Ukraine's state emergencies service DSNS in Kharkiv region

Takriban watu watatu wameuawa na wengine 17 kujeruhiwa katika shambulizi kubwa zaidi la ndege zisizo na rubani za Urusi kwenye mji wa pili kwa ukubwa wa Kharkiv nchini Ukraine, meya amesema.

Ihor Terekhov amesema kwamba usiku kucha Urusi ilirusha ndege zisizo na rubani 48, pamoja na makombora mawili ya kuongozwa kutoka mbali.

"Tuna kopo mkubwa," amesema, akiongeza kuwa majengo matatu ya ghorofa yalishambuliwa. Kanda za video zimeibuka zikionyesha ghorofa kadhaa za jengo moja kama hilo likiwaka moto.

Watu sita waliuawa na 80 kujeruhiwa kote Ukraine usiku uliopita , wakati Urusi ilishambulia nchi hiyo kwa zaidi ya droni 400 na karibu makombora 40.

Urusi ilisema kuwa nishati ya angani ilikuwa yakijibu "vitendo vya kigaidi vya Kyiv", ikidai kuwa maeneo ya kijeshi yalilengwa.

Hili limejitokeza siku chache baada ya shambulio la ndege zisizo na rubani za Ukraine zikilenga ndege za kimkakati za Urusi katika vituo vinne vya anga ndani ya nchi hiyo.

Soma zaidi:

Read Entire Article