Sancho

Chanzo cha picha, Getty Images

Dakika 3 zilizopita

Aston Villa imekuwa klabu ya hivi punde kuonyesha nia ya kumsajili winga wa Uingereza Jadon Sancho, 25, kutoka Manchester United. Sancho amekuwa akiichezea klabu ya Chelsea kwa mkopo.(Team Talk)

Newcastle United imemfanya mlinda lango wa Burnley na England James Trafford, 22, kuwa kipaumbele chao msimu huu wa kiangazi. (Times - usajili unahitajika)

Liverpool haina nia ya kumuuza winga wa Colombia Luis Diaz, 28, na haijapokea ofa, licha ya Barcelona na klabu ya Saudia Al-Nassr kumtaka. (Times - usajili unahitajika)