Israel inaendelea na mashambulizi dhidi ya Iran, jeshi lasema

21 hours ago 10

Fu Cong

Chanzo cha picha, Getty Images

China inalaani "ukiukaji wa Israel wa mamlaka, usalama na uadilifu wa ardhi ya Iran", mjumbe wa Umoja wa Mataifa Fu Cong alisema katika mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa saa chache zilizopita.

Beijing "ina wasiwasi mkubwa" juu ya athari mbaya ya hali ya sasa katika mazungumzo ya nyuklia ya Iran, aliongeza, akiitaka Israel kuacha mara moja hatua zote za kijeshi ili kuepuka kuongezeka zaidi.

Fu pia alisema kuwa haki ya Iran ya "matumizi ya amani ya nishati ya nyuklia kama mtia saini wa Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia inapaswa kuheshimiwa kikamilifu".

China ni mshirika mkuu wa Tehran, hasa katika nishati na miundombinu.

Mwezi Machi, China iliwakaribisha naibu mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Urusi mjini Beijing, ambapo walijadili suala la nyuklia la Iran na kuhimiza vikwazo dhidi ya Iran viondolewe.

Unaweza kusoma;

Read Entire Article