Iran yaanzisha tena mashumbulizi dhidi ya Israel

10 hours ago 5

.

Chanzo cha picha, EPA

Iran imefanya mashumbulizi mengine dhidi ya Israel, huku Televisheni ya taifa ya nchi hiyo ikisema kuwa imeanzisha "mashambulizi makubwa ya ndege zisizo na rubani".

Milipuko mikubwa imesikika katikati mwa Israel.

Video iliyothibitishwa na BBC pia inaonyesha moto ukiwaka karibu na kiwanda cha kusafisha mafuta cha Haifa nchini Israel kufuatia makombora yaliyorushwa kutoka Iran usiku wa kuamkia leo.

Mapema siku hiyo, runinga ya taifa ya Iran ilisema "zaidi ya makombora 100" yalirushwa Israel, yakilenga Haifa na Tel Aviv huku watu watatu wakifariki baada ya Iran kushambulia eneo la Bat Yam, pwani ya Israel, kulingana na huduma za dharura za Israel.

Waliofariki ni mwanamke mwenye umri wa miaka 69, mwanamke mwenye umri wa miaka 80 na mtoto wa miaka 10 wameuawa huko Bat Yam.

BBC haijaweza kuthibitisha hili kwa kujitegemea.

Kitongoji kimoja katika mji wa kaskazini wa Tamra pia kimeshambuliwa, na kuua takriban watu watano, vyombo vya habari vya Israel viliripoti huku hali ikisemekana kuwa bado ni tete.

Zifuatazo ni picha za hivi punde zinazotoka katika jiji la Tamra, katika Wilaya ya Kaskazini ya Israel.

.

Chanzo cha picha, Sinai Koren

,

Chanzo cha picha, Sinai Koren

,

Chanzo cha picha, Sinai Koren

Soma zaidi:

Read Entire Article