
YANGA inajiandaa kushuka uwanjani leo jioni kuvaana na Namungo ya Lindi, ikiwa ni mwendelezo wa mechi za Ligi Kuu Bara iliyoingia raundi ya 27, lakini ndani ya ofisi za mabosi wa klabu hiyo kuna mchakato wa maana unaendelea juu ya kusaka kocha mpya ajaye wakirusha kesho kwa kocha Mswisi.
Yanga imefanya mazungumzo ya awali na wasimamzi wa aliyekuwa kocha mkuu wa Al Ahly ya Misri, kocha Marcel Koller, raia wa Uswisi ili aje kuifundisha timu hiyo msimu ujao, ikielezwa timu hiyo ya Jangwani inajiandaa kuachana na kocha wa sasa, Miloud Hamdi.
Koller alilazimika kuingia makubaliano maalum na Ahly kufuatia kikosi hicho kutolewa katika hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa mshtuko na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini na kulitema taji ililokuwa inalishikilia.