
WAKATI kukiwa na taarifa kwamba Yanga ina mpango wa kuwa na benchi jipya la ufundi kwa msimu ujao, taarifa zinadai kuwa mabosi wa timu hiyo wameshaanza harakati za kusaka mbadala wa Kocha Miloud Hamdi.
Katika kumpata mbadala wa Hamdi, imeelezwa kuwa mabosi wa Yanga wametua Afrika Kusini kwa ajili ya kufanya mazungumzo na kocha Jose Luis Riveiro ambaye kwa sasa anaifundisha Orlando Pirates ya nchini humo.
Kupitia Mwanaspoti, iliwahi kuripoti kuwa kocha Jose huu ni msimu wake wa mwisho ndani ya Orlando Pirates kwani tayari amewaambia mabosi wa timu hiyo hataongeza mkataba utakapofikia tamati Juni 30, mwaka huu.