WHO laomba hospitali zilizosalia Gaza zilindwe

Shirika hilo limesema hospitali za Nasser na Al-Amal ziko hatarini kushindwa kufanya kazi kabisa kutokana na vizuizi vya misaada na barabara kufungwa, hali inayodhoofisha zaidi mfumo wa afya wa Gaza.

Kulingana na WHO, hospitali hizo tayari zimeelemewa na wagonjwa waliojeruhiwa vibaya ambao huletwa kila wakati, huku zikikabiliwa na upungufu mkubwa wa vifaa tiba.

Limesema ikiwa hospitali hizo zitafungwa, kutakuwa na athari kubwa na hasa kwa wagonjwa wa upasuaji, wagonjwa mahututi, wanaohitaji kuongezwa damu, wagonjwa wa saratani na wa figo.  

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *