Wanajeshi wa Israel wamuua mwanamke mjamzito wa Kipalestina na kichanga chake katika Ukingo wa Magharibi

Wanajeshi wa Israel wamemuua kwa kumpiga risasi mwanamke Mpalestina aliyekuwa na ujauzito wa miezi minane na kichanga kilichokuwa tumboni mwake wakati askari jeshi wa utawala huo ghasibu walipovamia kambi ya wakimbizi ya Nur Shams kaskazini magharibi mwa Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.