Waasi wa Tuareg: Jeshi la Mali limewaua raia 24 kaskazini mwa nchi

Muungano wa waasi wa Tuareg huko kaskazini mwa Mali umewatuhumu wanajeshi wa nchi hiyo kwa kuwaua raia 24 waliokuwa wakisafiri kuelekea kaskazini mwa Algeria kutoka mji wa Gao, huku jeshi likiripoti habari ya kujiri mapigano katika eneo hilo.