Vita vya Israel vyaacha mayatima 36,000 na wajane 14,000

Idadi ya watoto wa Kipalestina walioachwa yatima kutokana na vita vya siku 471 vya mauaji ya kimbari ya Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza imefikia zaidi ya 36,000, huku takriban wanawake 14,000 wakibakia baada ya waume zao kuuawa kufuatia hujuma na mashambulio ya kinyama ya Israel katika ukanda huo.