Uroho wa Trump katika muhula wa pili wa urais wake

Rais Donald Trump wa Marekani ameanza muhula wake wa pili wa uongozi huku akiweka hadharani uroho wake wa kupora ardhi, biashara na fedha za mataifa mengine ambapo ametangaza wazi azma yake ya kutaka kunyakua na kuunganisha ardhi za nchi huru na Marekani na pia kuhodhi kandarasi zenye faida kubwa kutoka kwa washirika wa Washington.