Umoja wa Mataifa: Watoto wa mwaka mmoja ni miongoni mwa waliobakwa Sudan

Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, watu wenye silaha wanabaka na kuwanyanyasa kingono watoto wenye umri hadi mwaka mmoja katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan.