
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky ametangaza kwamba angezungumza na Donald Trump leo Jumatano, Machi 19, siku moja baada ya mazungmzo ya simu kati ya rais wa Mrekani na Vladimir Putin, mazungumzo ambao yamefikia makubaliano ya usitishwaji mapigano kwa mud wasiku 30 kinyume na yale ambayo Washington ilikuwa ikiomba na Kyiv imekubali.
Imechapishwa:
Dakika 1
Matangazo ya kibiashara
Siku moja baada ya mazungumzo ya simu kati ya Vladimir Putin na Donald Trump, Volodymyr Zelensky, ambaye yuko katika ziara rasmi mjini Helsinki, ametangaza kwamba atakutana na rais wa Marekani siku ya Jumatano ili kujifunza zaidi kuhusu maudhui ya mazungumzo yao. Kwa kuongezea, Moscow na Kyiv zinapaswa kubadilishana wafungwa 175 wa vita kutoka kila upande wakati wa mchana. Fuata chanjo yetu ya moja kwa moja ya vita nchini Ukraine
“Leo nitawasiliana na Rais Trump, na tutajadili hatua zinazofuata,” Volodymyr Zelensky amesema katika mkutano na waandishi wa habari huko Helsinki.
Pia ametoa wito wa kutofanywa “makubaliano” kwa Urusi, ambayo inadai kukomeshwa kwa misaada ya Magharibi kwa Ukraine kabla ya usitishaji vita kwa ujumla. “Sidhani itakubalika kwa makubaliano yoyote katika suala la kusitishwa msaada kwa Ukraine, lakini kinyume chake, misaada inapaswa kuongezwa kwa Ukraine,” amesema.
Putin alimwambia Trump usitishaji kamili wa mapigano utafanya kazi tu ikiwa washirika wa Ukraine wataacha kutoa msaada wa kijeshi – hali ambayo washirika wa Ukraine wa Ulaya wamekataa hapo awali.
Hayo yanajiri wakati rais Vladimir Putin amekataa usitishaji vita wa mara moja na kamili nchini Ukraine, akikubali tu kusitisha mashambulizi kwenye miundombinu ya nishati, kufuatia mazungumzo yake na Rais wa Marekani Donald Trump.
Tarehe ya mazungumzo yajayo kati ya Urusi na Marekani kutangazwa katika siku zijazo, kulingana na Kremlin
Msemaji wa Kremlin ametangaza kwamba tarehe ya mazungumzo mapya kati ya Urusi na Marekani itajulikana katika siku zijazo.
Dmitry Peskov amebaini wakati wa mkutano wake wa kila siku na waandishi wa habari kwamba majadiliano yamepangwa kwa siku ya Jumatano na Alhamisi ili kuamua “tarehe sahihi za mazungumzo yanayofuata na muundo” wa wajumbe wa Urusi na Marekani.