Uganda yatuma vikosi zaidi nchini DRC, yathibitisha kuwa wanajeshi wake wameingia Bunia

Msemaji wa Jeshi la Uganda Brigedia Jenerali Felix Kulayigye amethibitisha kuwa Jeshi la Ulinzi la nchi hiyo (UPDF) limeingia kwenye eneo la Bunia, ambalo ni makao makuu ya jimbo la Ituri, sehemu muhimu ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC.