Uganda inasema imetuma wanajeshi wake Sudan Kusini, Juba yakanusha

Uganda imetuma wanajeshi wake jijini Juba, nchini Sudan katika kile mkuu wa majeshi ya nchi hiyo Muhoozi Kainerugaba, amesema wamekwenda kulinda usalama, kuepusha kutokea machafuko mapya, hasa wakati huu ambao rais Salva Kiir na makamu wake Riek Machar wakionekana kutofautiana.

Imechapishwa: Imehaririwa:

Dakika 1

Matangazo ya kibiashara

Haya yanajiri baada ya  Mvutano kuzidi kati ya Kiir na Naibu wake Riek Machar, na kuzua hofu kuwa makubaliano yao ya mkataba wa amani wa mwaka 2018 huenda yakaysambaratika na nchi kurejea kwenye  vita.

Hata hivyo  Jenerali Kainerugaba hajatoa maelezo kwa nini Uganda imeamua kutuma vikosi vyake katika nchi hiyo Jirani lakini ameonya tishio lolote la  kumuondoa Salva Kiir ni sawa na kutangaza vita dhidi ya Uganda.

Sudan  Kusini haijazungumzia tangazo hilo la kupata msaaada wa kijeshi kutoka Uganda.

Inahofiwa kwamba huenda kukawa na mpasuko kwenye serikali kati ya upande wa rais Salva Kiir na ule wa Riek Machar.
Inahofiwa kwamba huenda kukawa na mpasuko kwenye serikali kati ya upande wa rais Salva Kiir na ule wa Riek Machar. © Ben Curtis / AP

Wiki iliyopita, Naibu Mkuu wa Jeshi la Sudan Kusini pamoja na mawaziri wawili, wote ni washirika wa Machar, walikamatwa na vikosi vya usalama.

Kukamatwa kwa viongozi hao kulifuatia  mapigano katika jimbo la Upper Nile kati ya vikosi vya serikali na waasi wa White Army, ambao walikuwa washirika wa karibu wa Machar wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilizuka 2013 baada ya mivutano ya madaraka kati yake na Kiir.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *