
Katika chapisho kwenye ukurasa wake mtandao wa kijamii wa X saa chache baada ya timu za wawakilishi wa Marekani na China kukamilisha mazungumzo ya siku mbili mjini London, Trump alisema makubaliano hasa yanasubiri kuidhinishwa na yeye na Rais wa China, Xi Jinping.
Mazungumzo ya biashara kati ya Marekani na China kuendelea, baada ya “simu” ya Trump na Xi
Tangu Trump aanzishe vita vya biashara na China mwezi Februrari, mataifa hayo mawili yenye uchumi mkubwa zaidi duniani yamekuwa katika mvutano wa kupandishiana ushuru ambao umevuruga masoko ya dunia.