Tetesi za soka Ulaya Ijumaa 26.07.2024

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Dani Olmo

Manchester City wametoa ofa thabiti kumsajili kiungo wa kati wa Uhispania Dani Olmo, 26, kutoka RB Leipzig. (Foot Mercato – In French)

Barcelona pia wametuma ofa yenye thamani ya zaidi ya £50m kwa Olmo. (Sky Sports)

Beki wa Uingereza Jarrad Branthwaite, 22, ana nia ya kutosaini mkataba mpya Everton isipokuwa iwapo wanaweza kufikia pauni 160,000 kwa wiki zinazotolewa na Manchester United. (Mail)

Beki wa Manchester United Muingereza Aaron Wan-Bissaka, 26, amekataa ofa kutoka kwa West Ham na angependelea kuhamia Inter Milan msimu huu. (Sportsport)

Mipango ya Brentford ya kumwachia Ivan Toney anayelengwa na Tottenham na West Ham kuondoka katika klabu hiyo inaweza kusitishwa baada ya mshambuliaji wa Uingereza Igor Thiago, 28, kupata jeraha katika mechi za kabla ya msimu mpya. (Sun)

Pia unaweza kusoma
.

Chanzo cha picha, PA Media

Maelezo ya picha, Ivan Toney

Crystal Palace wamekubali mkataba wa euro 15m (£12.6m) kimsingi kumsaini winga wa Senegal Ismaila Sarr, 26, kutoka Marseille. (Athletic – Subscription required)

Kiungo mshambuliaji wa Arsenal na Uingereza Emile Smith Rowe anakaribia kujiunga na Fulham baada ya Mikel Arteta kumwacha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 kwenye mechi ya kirafiki ya kujiandaa na msimu mpya dhidi ya Bournemouth nchini Marekani. (Guardian)

Aston Villa inamfuatilia winga wa Borussia Dortmund na Ujerumani Karim Adeyemi, 22, ambaye pia amewavutia Juventus na Chelsea. (Mail)

Winga wa Napoli na Denmark Jesper Lindstrom, 24, amekamilisha vipimo vyake vya afya katika klabu ya Everton. (Fabrizio Romano)

.

Chanzo cha picha, Getty

Maelezo ya picha, Kepa

Kipa wa Chelsea Mhispania Kepa Arrizabalaga mwenye umri wa miaka 29 anaweza kubadilishana nafasi na mlinda mlango wa Real Madrid mwenye umri wa miaka 25 Andriy Lunin katika makubaliano ya kubadilishana kati ya klabu zote mbili. (AS – In Spanish)

West Ham wamewasilisha ombi la pauni milioni 30 na kumpa kiungo wa kati wa Uingereza Lewis Orford mwenye umri wa miaka 18 katika harakati za kumsajili mshambuliaji wa Aston Villa na Colombia Jhon Duran, 20. (Athletic – subscription required)

Nottingham Forest imekataa ombi la West Ham la kumnunua beki wa pembeni wa Wales Neco Williams, 23. (HITC)

.

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Joao Neves

Chelsea wanakaribia kumsajili mlinzi wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 21 Guela Doue kutoka Rennes kwa mkataba wa £7.6m. (Sky Italia)

Paris St-Germain wanakaribia kukamilisha dili la kiungo wa kati wa Benfica na Ureno Joao Neves, 19. (Fabrizio Romano)

Winga wa Paraguay Miguel Almiron, 30, yuko kwenye mazungumzo ya juu ya kuondoka Newcastle kwa klabu ambayo haijatajwa jina ya Saudi Pro League. (Football Insider)

Pia soma

Imetafsiriwa na kuchapishwa na Seif Abdalla