Spika wa bunge la Algeria ataka kujinaishwa ukoloni wa Ufaransa nchini humo

Spika wa Bunge la Algeria, Ibrahim Boughali ametoa mwito wa kupasishwa sheria inayojinaisha ukoloni wa Ufaransa na kuutambua rasmi kuwa ni uhalifu. Mwito huo ni kiashiria tosha cha kuongezeka mvutano kati ya Algeria na mkoloni kizee wa Ulaya yaani Ufaransa.