Rwanda yajiondoa katika Jumuiya ya ECCAS

Hatua hiyo imekuja baada ya viongozi wa ECCAS kuongeza muda wa rais wa Jumuiya hiyo kutoka Equatorial Guinea kwa mwaka mwengine mmoja, ikiipita Rwanda iliyokuwa ichukua kijiti hicho cha uongozi. 

Waasi wa M23 ambao wataalamu wa Umoja wa Mataifa na Marekani wanasema Rwanda inaendelea kuwaunga mkono, wamedhibiti miji muhimu Mashariki mwa Kongo tangu mwezi Januari mwaka huu katika mapigano ambayo yamesababisha mauaji ya maelfu ya watu. 

Rwanda yajiunga na ukosoaji wa utawala mbadala wa M23

Kulingana na kamishna wa ECCAS ambae hakutaka kutajwa jina, kulikuwa na mvutano mkali kati ya mawaziri wa Rwanda na Kongo, na upande wa Kongo ulionya kwamba hautaweza kusafiri kuelekea Rwanda kwa mikutano ya Jumuiya hiyo iwapo Rwanda itaiongoza. 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *