Ramadhani imeanza na mgogoro wa vita unaendelea nchini Sudan

Sambamba na kuanza mwezi mtukufu wa Ramadhani, Jeshi la Sudan SAF limezidisha mashambulizi ya kuuteka kikamilifu mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum, kutoka mikononi mwa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF). Hata hivyo kampeni hiyo inasababisha hasara kubwa hasa kwa watoto wa nchi hiyo. Mapigano hayo yamesambaratisha maisha ya vijana na kushadidisha njaa, mbali na janga la majeruhi, wajane na mayatima.