Rais wa Marekani anataka kunyakua Ukanda wa Gaza

Katika taarifa isiyo na mfano wake na ya ghafla, Rais wa Marekani amesema mbele ya Waziri Mkuu wa Israel huko White House kwamba Marekani inanuia kuutwaa Ukanda wa Gaza na pia kuwa kuna uwezekano wa nchi hiyo kutambua rasmi udhibiti wa utawala wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.