Rais Pezeshkian arejea Tehran baada ya kutembelea Tajikistan na Russia

Rais Masoud Peshkeskian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye alikuwa kwenye ziara za kikazi za kutembelea Dushanbe na Moscow akiongoza ujumbe wa ngazi za juu kwa mwaliko rasmi wa Marais Emomali Rahmon wa Tajikistan na Vladimir Putin wa Russia, amerejea hapa Tehran mapema leo Jumamosi.