
Zaidi ya Warundi milioni 6 hii leo Juni 5 wanaamikia katika vituo zaidi ya 14,000 vya kupigia kura, ili kuwachagua wabunge wao na madiwani wa manispaa, katika hali mbaya ya mazingira ya nchi iliokumbwa pakubwa na mgogoro wa kiuchumi pamoja na uhaba wa bidhaa mbalimbali, huku ikionekana tayari mshindi anafahamika.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Baada ya wiki tatu za kampeni zilizotawaliwa na chama tawala cha CNDD-FDD, ambacho kimetawala nchi hiyo kwa mkono wa chuma tangu mwaka 2005, hii leo sasa ndio siku yenyewe ya upigaji kura.
Huu ni uchaguzi wa kwanza wa wabunge na viongozi wa manispaa kutofanyika kwa wakati mmoja tofauti na uchaguzi wa rais, kwa mujibu wa katiba mpya ya Burundi iliyopitishwa mwaka 2018, ambayo iliongeza muda wa uongozi wa mkuu wa nchi hadi miaka saba, huku ule wa wabunge na madiwani wa manispaa ukibaki miaka mitano.
Jambo lingine jipya ni kwamba idadi ya majimbo ya uchaguzi wa wabunge imepunguzwa kutoka 18 hadi matano, bado kwa mujibu wa katiba mpya ya nchi, wakati idadi ya wabunge waliochaguliwa haikubadilishwa.
Wapiga kura lazima wachague wabunge 100, asilimia 60% kati yao wakiwa Wahutu walio wengi na asilimia 40% kutoka kwa Watutsi walio wachache, na takriban asilimia 30% ya wanawake.
Kwa uchaguzi wa manispaa, idadi ya manispaa imepunguzwa kutoka 119 hadi 42, lakini hakuna tena mgawo wa kikabila uliowekwa kwa vyama vya siasa, kama zamani.
Leo, Warundi walio katika umri wa kupiga kura watalazimika kuchagua kati ya wagombea kutoka chama cha CNDD-FDD, ambacho kimekuwa madarakani kwa miaka 20, na vyama vidogo.
Pia, kutakuwa na wagombea wachache wa kujitegemea, bila ya kiongozi mkuu wa upinzani, Agathon Rwasa, na wafuasi wake, ambao wamezuiwa kushiriki katika uchaguzi huo kwa hila zilizopangwa na serikali, ambayo wanadai serikali inakanusha.