Raia katika Mji wa El-Fasher Sudan wakabiliwa na hali mbaya ya kibinadamu

Raia walionaswa katika mapigano kwenye mji wa El-Fasher nchini Sudan, wanakabiliwa na hali mbaya ya kibinadamu, wameonya watetezi wa haki za binadamu ambao wamesema hali kwenye mji huo inazidi kuwa mbaya kufuatia miezi kadhaa ya mashambulio ya wapiganaji wa RSF.

Imechapishwa:

Dakika 1

Matangazo ya kibiashara

Kulingana na ripoti ya kundi la kutetea haki za binadamu  the Darfur General Coordination of Camps for the Displaced and Refugees, raia wa eneo hilo la Elfasher wanakikabiliwa na njaa,magonjwa na ukame wakati huu milio ya makombora na mizinga ikisikika eneo hilo.

Tangu Aprili mwaka wa  2023 Vikosi vya RFS  vimechukua sehemu kubwa ya eneo  la Darfur isipokuwa eneo la  El-Fasher  liliko Darfur Kaskazini huku bei za bidhaa zikiogezeka na ukosefu wa pesa ukishuhudiwa .

Makundi yanayounga mkono  RSF  Sudan Liberation Army na the Gathering of Sudan Liberation Forces  mwishoni mwa juma yalitoa  wito kwa raia wa  El-Fasher na kambi zilizo karibu za Abu Shouk na Zamzan kuondoka, na kuonya kuongezeka kwa operesheni za kijeshi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *