Pezeshkian: Mataifa ya Kiislamu yaungane kuijenga upya Gaza

Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian ametoa mwito kwa nchi za Kiislamu kuungana na kushirikiana ili kulijenga upya eneo la Ukanda la Gaza ambalo limeharibiwa kikamilifu na mabomu ya utawala wa Kizayuni wa Israel.