
ACHANA na stori inayotrendi kwa sasa juu ya Yanga kugomea kucheza mchezo wa Dabi ya Kariakoo dhidi ya watani zao, Simba, ikisisitiza tena kwamba haina mpango wa kucheza mechi hiyo hata kama itapangwa na Bodi ya Ligi, lakini kuna mambo mbalimbali yanayohusiana na mastaa wa timu hiyo.
Tayari Yanga imeshakata tiketi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao kutokana na nafasi iliyopo kwa sasa, na mabosi wa timu hiyo wameishaingia chimbo kuweka mambo sawa ili mashindano yatakapoanza chama hilo likiwashe na kurejesha heshima yake ngazi ya kimataifa.