Orodha ya mazungumzo kuhusu vita vya Gaza tangu Oktoba 7 hadi sasa

Qatar inahodhi mazungumzo ya kusitisha mapigano huko Gaza siku ya Alhamisi, ikitarajia kufikia makubaliano ambayo yatazuia Iran kufanya mashambulizi dhidi ya Israel ambayo yatapanua mzozo huo.

Marekani, Misri na Qatar zimetoa wito kwa Israel na Hamas kufanya mazungumzo ya kusitisha vita vilivyodumu kwa zaidi ya miezi kumi.

Mapema Oktoba 7, vita hivi vilizuka wakati wanamgambo wa Hamas waliposhambulia maeneo ya Israel huko Gaza, na kuua takribani Waisraeli 1,200 na kuwateka nyara wengine 240. Israel ilijibu katika kampeni inayoendelea hadi leo, ikigharimu maisha ya Wapalestina wapatao 40,000 na kujeruhi makumi ya maelfu.