Netanyahu: Saudia imege ardhi yake na kuwapatia Wapalestina waunde nchi yao

Waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amependekeza Wapalestina waunde nchi yao ndani ya Saudi Arabia badala ya kwenye ardhi ya nchi yao ya asili; na ametupilia mbali dhana yoyote ya kuwepo nchi ya Palestina yenye mamlaka kamili ya kujitawala.