Museveni apuuza uamuzi wa mahakama juu ya mahakama za kijeshi

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni amesema serikali yake itaendelea kuwashtaki raia katika mahakama za kijeshi, licha ya Mahakama ya Juu ya nchi hiyo kupiga marufuku hatua hiyo, ikisema ni kinyume cha katiba.