Mkutano wa Jeddah; licha ya kukamilisha lakini ni zaidi ya mkutano wa Cairo

Kufanyika mkutano wa dharura wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Kiislamu huko Jeddah mara baada ya mkutano wa dharura wa mawaziri wa Mambo ya Nje na Wakuu wa Nchi za Kiarabu huko Cairo, Misri kunaonyesha ushirikiano wa pamoja wa Ulimwengu wa Kiislamu katika kukabiliana na mpango wa kuwafukuza kwa nguvu wakazi wa Ukanda wa Gaza na wa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.