
Trump ameandika kupitia mtandao wake wa kijamii wa Truth Social kwamba wamejadiliana kwenye mazungumzo hayo ya simu kuhusiana na masuala kadhaa hususan kuhusu ya utata kwenye Makubaliano ya Kibiashara uliojitokeza hivi karibuni.
Rais huyo wa Marekani amesema mazunguzo hayo yaliyodumu kwa saa moja na nusu yamekuwa na matokeo mazuri sana kwa mataifa yote mawili.
Aidha, Trump amesema Xi amemwalika yeye na mkewe Melania kuzuru China, ombi ambalo pia Trump alimtolea Jinping na kwa ujumla wote wawili wamekubali kutembeleana.