Marekani yawaamuru maafisa wake kuondoka Mashariki ya Kati

Shirika la habari la Reuters linaripoti kwamba Marekani inajitayarisha kuwaondosha maafisa wake wa ubalozi nchini Iraq na kuziruhusu familia za wanajeshi kuondoka kote Mashariki ya Kati kutokana na kitisho kikubwa cha usalama, kwa mujibu wa vyanzo ndani ya Marekani na Iraq kwenyewe.

Soma zaidi: Iran yatishia kushambulia kambi za Marekani iwapo patatokea mgogoro kati yake na taifa hilo

Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imewaruhusu pia wale wanaotaka kuondoka kwa khiyari nchini Bahrain na Kuwait kufanya hivyo.

Uamuzi huu umechukuliwa wakati juhudi za kufikia makubaliano juu ya mpango wa nyuklia wa Iran zikionekana kukwama, na taarifa za kijasusi za Marekani zikiashiria kuwa Israel imekuwa ikijitayarisha kuvishambulia vinu vya nyuklia vya Iran, hatua inayoweza kuifanya Tehran kulipiza kisasi. 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *