Mamlaka ya Ndani ya Palestina yataka walimwengu waishinikize Israel

Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina imeonya juu ya matokeo mabaya ya kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia Gaza na kuitaka jamii ya kimataifa kuulazimisha utawala wa Kizayuni utekeleze majukumu yake ya kibinadamu.