Mali yasitisha vibali vya uchimbaji madini kwa wageni

Waziri wa Usalama na Ulinzi wa Raia wa Mali, Daoud Aly Mohammedine ametangaza rasmi kwamba: Vibali vyote vya uchimbaji madini nchini Mali vilivyotolewa kwa watu wenye uraia wa kigeni vimesitishwa kwa amri ya Rais Assimi Goïta wa Mali.