
Msafara wa magari ya jeshi la Mali na Africa Corps—mamluki wa Urusi waliochukuwa nafasi ya kundi la Wagner—umeshambuliwa siku ya Ijumaa, Juni 13, na waasi wanaotaka kujitenga wa FLA (Azawad Liberation Front) kati ya Anefis na Aguelhoc, kaskazini mwa nchi. FLA imedai “ushindi mkubwa.” Jeshi la Mali, baada ya kukanusha shambulio lolote, limedai kupata ushindi.
Imechapishwa:
Dakika 2 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Msafara wa jeshi na Africa Corps, mamluki wa Urusi ulikuwa na magari zaidi ya thelathini—magari ya kivita, lori, gari, na magari mengine, na yalikuwa yanasheheni chakula. Msafara huo ulilengwa kwa mara ya kwanza siku ya Alhamisi, Juni 12, kwa mabomu yaliyotengenezwa kienyeji huko Tadjereret. Siku ya Ijumaa asubuhi, huko Anoumalane, yapata kilomita arobaini kutoka Aguelhoc, Kikosi cha Ukombozi cha Azawad kilivizia msafara huo, hasa kwa silaha nzito, kwa zaidi ya saa mbili. Jeshi la Mali hatimaye lilijibu kwa mashambulizi ya angani—ndege zisizo na rubani, ndege za kivita na helikopta zilitumwa—jambo ambalo lilizima mapigano hayo. Vita hivyo vilifanyika kwa mbali, bila mapigano ya karibu.
Wanachama kadhaa wa ALF, pamoja na vyanzo vya usalama na raia wa Mali, wamethibitisha kuwa magari mengi ya kijeshi yaliharibiwa. ALF imeelezea tukio hilo kama “ushindi mkubwa,” ikisisitiza kwamba magari mengi “yaliteketezwa kwa moto,” na kwamba “maadui” wengi waliuawa, bila kutoa maelezo juu ya utambulisho wao – askari wa Mali au wapiganaji wa Kirusi kutoka Africa Corps. ALF pia imedai kupata takriban magari kumi na tano, ikiwa ni pamoja na gari la kivita na lori kumi na mbili. Waasi hao walitoa picha za magari mengi yaliyoharibiwa au kuibiwa.
Jeshi la Mali labadilisha toleo lake
Katika taarifa ya awali iliyochapishwa mapema Ijumaa alasiri, jeshi la Mali awali lilikanusha “shambulio lolote lililodaiwa” na kukashifu “taarifa za uwongo” zilizokusudiwa “kuzua hofu na kuvuruga maoni ya umma.” Saa mbili baadaye, taarifa mpya kutoka kwa makao makuu ya jeshi badala yake ilidai kushindwa mara mbili kwa “kundi la kigaidi lenye silaha,” na “shambulio” siku ya Alhamisi na kutoa “jibu la haraka” siku ya Ijumaa.
Vifo hivyo vinaaminika kuwa kati ya dazeni, lakini hakuna takwimu za kuaminika ambazo zimethibitishwa bado. Ripoti zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zikiripoti helikopta iliyotunguliwa na wapiganaji wa Africa Corps kukamatwa hazina msingi.
Takriban mwaka mmoja uliopita, Julai 2024, kundi la Wagner lilipata hasara kubwa baada ya kushindwa kwa kiasi kikubwa huko Tinzaouatène. Kundi hilo lilipoteza wapiganaji zaidi ya 80. Wakiwa wametua tu, warithi wao Africa Corps walmepata pigo lao la kwanza katika jimbo hilo la Kidal.