
Nchini Mali, hali ya utulivu inatawala katika eneo la kaskazini kufuatia mapigano ya siku ya Ijumaa, Juni 13, kati ya muungano wa Jeshi la Mali/Africa Corps (zamani Wagner) na waasi wa Mali wa Azawad Liberation Front (ALF). Waasi, ambao wanadai kuwa walianzisha “shambulio la jumla kaskazini,” walitangaza kuwa waliidungua ndege ya muungano. Mamlaka badala yake inarejelea ajali inayohusiana na hali ya hewa.
Imechapishwa:
Dakika 1 Wakati wa kusoma
Matangazo ya kibiashara
Na mwandishi wetu wa kikanda, Serge Daniel
Ndege hiyo ilianguka na kuwaka moto karibu na uwanja wa ndege wa Gao, mji mkuu kaskazini mwa Mali. Ilikuwa ndehe aina ya Sukhoi iliyotengenezwa na Urusi. Marubani wawili, pia Warusi, wako salama. Waendesha meli walisafirisha miili hiyo. Video zilizoidhinishwa zinaonyesha wapiganaji wa Ursi Africa Corps, silaha zikiwa zimetundikwa mabegani mwao, wakilinda mabaki ya ndege hiyo. Kwa mujibu wa jeshi la Mali, mazingira mabaya ya hewa ndiyo iliyosababisha kutunguliwa kwa ndege hiyo.
“Uongo,” wanajibu waasi wa Mali wa kundi la Ukombozi wa Azawad (ALF). Wanadai kuitungua ndege hiyo, kwa mujibu wa msemaji wa ALF Mohamed el-Maouloud Ramadan: “Tunathibitisha kuwa ni ALF iliyoiangusha ndege leo. Ni moto wa ALF uliosababisha kuangushwa kwa ndege hii.”
Ameongeza kuwa waasi wa kundi la Ukombozi la Azawad wanaanzisha mashambulizi ya jumla.
Jeshi la Mali, kwa upande wake, katika taarifa zake zilizochapishwa hivi punde, linadai kuwa hali inadhibitiwa kote nchini.