MAANDALIZI YA MKUTANO MAALUM CCM TAIFA YAIVA JIJINI DODOMA

MAANDALIZI YA MKUTANO MAALUM CCM TAIFA YAIVA JIJINI DODOMA
KATIBU  wa Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Taifa, CPA Amos Makalla,akizungumza na waandishi wa habari leo Mei 24,2025 jijini Dodoma kuelekea Mkutano  Mkuu maalumu  wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa  unatarajiwa kufanyika Mei 29-30 katika ukumbi wa Jakaya Conversion na utahudhuriwa na wajumbe wa mkutano Mkuu kutoka maeneo mbalimbali.
KATIBU  wa Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Taifa, CPA Amos Makalla,akijibu maswali mbalimbali yaliyoulizwa  na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuelekea Mkutano  Mkuu maalumu  wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa  unatarajiwa kufanyika Mei 29-30 katika ukumbi wa Jakaya Conversion.
Na.Alex Sonna-DODOMA
MAANDALIZI kwa ajili ya mkutano Mkuu maalumu  wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa   yamekamilika na  unatarajiwa kufanyika Mei 29-30 katika ukumbi wa Jakaya Conversion na utahudhuriwa na wajumbe wa mkutano Mkuu kutoka maeneo mbalimbali.
Katibu wa Itikadi,Uenezi na Mafunzo CCM Taifa, CPA Amos Makalla,ameyasema hayo leo Mei 24,2025 jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuelekea Mkutano huo.
“Tunauhakika tutaweka historia ya kuwa na mkutano wa kipekee kuvunja historia ya ule uliopita,maandalizi yamekamilika hata nyie Waandishi mnaona ukumbi unaendelea kupambwa sisi kila siku tunataka kufanya mambo ya kihistoria,”amesema CPA Makalla.
Aidha amesema kuwa mkutano huo utatanguliwa na kikao cha kamati  Kuu ambacho  kitafanyika  Mei 26 na kisha Halmashauri Kuu Mei 28 .
Katika hatua nyingine,Makalla amesema kuwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano,Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuweka Jiwe la Msingi la Jengo la Makao Makuu ya CCM Mei 28 mwaka huu.
Amesema kuwa Jengo hilo litakuwa la kisasa ambalo litakuwa na huduma zote muhimu na litaendana na hadhi ya CCM ambayo kwa sasa inawanachama zaidi ya milioni 11.
“Tunajenga jengo la Makao Makuu pembeni ya Jengo hili ( Jakaya Conversion) ambalo litakuwa na facilities zote CCM ni Chama kikubwa Tanzania pamoja na Afrika,tumeona umefika wakati wa kuwa na jengo lenye facilities zote kumbi za mkutano, parking kwa sababu  Chama hichi ni kimbilio la  wananchi,”amesema  Makalla.
Aidha amesema kuwa mkutano huo utakuwa na agenda tatu ambazo ni kupokea taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM katika kipindi cha miaka mitano kwa Serikali zote mbili,uzinduzi wa ilani ya uchaguzi 2025-2030 na marekebisho madogo ya katiba.
“Nitumie fursa hii kuwaalika wajumbe wote wa mkutano Mkuu karibuni Dodoma mambo yote yamekamilika tunawakaribisha hata ambaye sio mwananchi  hata kama hujaalikwa unakaribishwa pia tutaweka eneo maalumu kwa ajili ya kuangalia,”amesema

The post MAANDALIZI YA MKUTANO MAALUM CCM TAIFA YAIVA JIJINI DODOMA appeared first on Mzalendo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *