Maafisa wa SADC na EAC watilia mkazo kusitishwa mapigano mashariki mwa Kongo

Maafisa wa ngazi ya juu kutoka mataifa ya Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika jana walitilia mkazo kusitishwa mara moja mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kuzitaka pande zote husika kutoa kipaumbele kwa suala la kufanya mazungumzo ili kuupatia ufumbuzi mgogoro uliopo.