Kusini mashariki mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati yatikiswa na mlipuko mpya wa ghasia

Wapiganaji kutoka jamii ya Zande, waliokuwa wametia saini makubaliano ya kujiunga na jeshi la Jamhuri ya Afrika ya Kati na kupewa mafunzo na mamluki wa Urusi mwaka mmoja uliopita, wamechukua silaha tena katika eneo la Haut-Mbomou. Kwa wiki moja, wamekuwa wakiwashambulia wanajeshi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na mamluki wa Urusi kutoka Wagner katika maeneo ya Zemio na Mboki.

Imechapishwa:

Dakika 1

Matangazo ya kibiashara

Mnamo Mei 1, 2024, takriban wapiganajizaidi ya mia moja wa kundi la kujilinda cla Azande Ani Kpi Gbe walivaa sare mpya za jeshi la Jamhuri Afrika ya Kati chini ya usimamizi wa mamluki wa Urusi waliotumwa katika eneo hilo hivi karibuni ili kutuliza vurugu. Lakini mwaka mmoja baadaye, makubaliano hayo yamevurugika: uvivu uliwarudisha wanamgambo wengi msituni, na baada ya wiki za mvutano, walilenga wanajeshi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati (FACA) na wakufunzi wao wa zamani wa Wagner mnamo Aprili 30 na siku zilizofuata.

Kulingana na vyanzo kadhaa, hatua hii inaweza kuelezewa kwanza na ongezeko la ukamataji ndani ya jamii ya Wazande, wakiwemo machifu wa vijiji na viongozi wa vitongoji vinavyokumbwa na vurugu. Lakini sababu zake pia zina mwelekeo wa kiuchumi, katika kesi hii makubaliano kati ya Warusi na viongozi wa makundi ya Fulani yenye silaha yanayosimamia ufugaji wa mifugo.

Visa vya uporaji na uchomaji moto wa nyumba vyaripotiwa Mboki

Kulingana na Umoja wa Mataifa, hali hiyo tayari imesababisha watu 10,000 kuyahama makazi yao, nusu yao wakiwa wamevuka Mbomou na kuingia DRC.

Baada ya utulivu huko Zémio, ni eneo la Mboki, karibu kilomita mia moja, ambalo limekumbwa na mapigano tangu jioni ya Jumanne Mei 6, na visa vya uporaji na nyumba kuchomwa moto ambavyo pia vinaripotiwa vimesababisha watu waliolazimika kuhama makazi yao kuwa wengi. Hakuna idadi ya watu wanaoaminika kutokana na vurugu hii inayoendelea kwa sasa.

Kwa upande wake, MINUSCA, kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, kimekanusha operesheni yoyote ya pamoja na Wagner baada ya kundi hilo la mamluki kuchapisha picha za wanajeshi wake wakiwa na walinda amani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *