Kugonga mwamba mpango wa Serikali ya Marekani wa kuiwekea vikwazo ICC

Baraza la Seneti la Marekani halijauidhinisha mswada wa vikwazo dhidi ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, vikwazo ambavyo ni jibu la utoaji vitisho linalolenga kuiadhibu mahakama hiyo kwa uamuzi wake wa kutoa hati za kukamatwa waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na aliyekuwa waziri wa vita wa utawala huo wa Kizayuni Yoav Gallant.