
KOCHA Mkuu wa Fountain Gate Princess, Camil Mirambo amesema malengo ya timu hiyo msimu huu ni kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi.
Timu hiyo iko nafasi ya saba kwenye msimamo na katika mechi 13, imeshinda nne, sare mbili na kupoteza saba ikikusanya pointi 14.
Akizungumza na Mwanaspoti, Mirambo alisema wana nafasi ya kumaliza nafasi ya nne kwenye msimamo licha ya ugumu wa mechi tano zilizosalia na timu wanazowania nafasi hiyo.