Kocha afichua jambo KenGold

BAADA ya KenGold kushuka Ligi Kuu ikiwa na mechi tatu mkononi, kocha Omary Kapilima ametaja mambo mawili yaliyowaangusha, huku akisisitiza wanajipanga kurudi msimu ujao.

KenGold imerudi Championship baada ya kupanda msimu huu na kushindwa kuonja nafasi nzuri katika msimamo, kwani tangu imepanda hadi inashuka ilikuwa nafasi ya mwisho.

Akizungumza na Mwanaspoti, Kapilima alisema wameangushwa na ugumu wa ligi na pia usajili mbaya wa mzunguko wa kwanza ambao waliamini kikosi kilichowapandisha kingeonyesha ushindani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *