Kansela Merz asema ameridhika na mazungumzo na Trump

Akizungumza na DW muda mfupi baada ya mazungumzo yake na Trump mjini Washington, Kansela Merz amesema amemkumbusha Trump kwamba Marekani wakati wote itabaki kama kiongozi wa ulimwengu katika jitihada za kuyashinikiza mataifa yanayoingia vitani.

Kansela Merz aidha amesema suala jingine kubwa walilojadiliana ni ushuru akisema, amejaribu kumshawishi Trump na serikali yake kwamba wanatakiwa kuzungumza ili kupata suluhisho, ingawa amesema hilo litachukua muda.

Aidha amesema Trump amekubali mwaliko wa kuitembelea Ujerumani na tayari timu inayohusika imeanza kuandaa tarehe ya ziara hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *