Kamanda: Jeshi la Iran linabadilisha mbinu za kukabiliana na vitisho

Kamanda mwandamizi wa Iran amesema Iran itabadilisha mbinu na mikakati yake ya kijeshi ili kukabiliana na vitisho vinavyobadilika. Kamanda wa Kikosi cha Ulinzi wa Anga cha Jeshi la Iran, Brigedia Jenerali Alireza Sabahi-Fard, ameyasema hayo Jumamosi na kuongeza kuwa maadui na wavamizi hawawezi kufikia anga ya Iran.