
JKU kutoka Unguja imetinga fainali ya Kombe la Muungano baada ya kuifunga Azam mabao 2-1, huku kocha wa timu hiyo, Haji Ali Nuhu akisema wanataka kubeba ubingwa.
Akizungumza na Mwanaspoti, kocha huyo alisema ushindi dhidi ya Azam ni mkakati waliojiwekea ili kutinga fainali.
Alisema ingawa mchezo unaofuata wa fainali utakuwa mgumu zaidi, lakini kutokana na maandalizi watakayoyafanya watahakikisha wanaondoka na ubingwa.