
Siku ya Jumanne, afisa mwandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, ambaye hakutaka kutajwa jina, aliliambia shirika la habari la TRT World kwamba uwezekano wa Marekani kushiriki katika mashambulizi ya kijeshi dhidi ya maeneo ya nyuklia ya Iran unazidi kuzingatiwa.
“Chaguo hilo linatazamwa kwa umakini,” alisema afisa huyo. “Hata hivyo, uamuzi wa mwisho unategemea Ikulu ya White House. Maamuzi hayo hufanywa huko.”