
Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty amehimiza kusitishwa mara moja mapigano kati ya Iran na Israel katika mazungumzo mawili tofauti ya simu na mjumbe wa Marekani Mashariki ya Kati Steve Witkoff na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araqchi.
Abdelatty alisisitiza umuhimu wa kurejea kwenye mazungumzo kama njia pekee ya kufikia makubaliano endelevu kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran, kulingana na taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya Misri.
Nchini Iran, takriban watu 224 wameuawa tangu uhasama uanze siku ya Ijumaa. Huku takriban watu 24 wameuawa Israeli.