
Awali, mkutano huo uliitishwa kwa lengo la kushughulikia changamoto kadhaa vikiwemo vita kati ya Urusi na Ukraine lakini ukagubikwa na mzozo wa Mashariki ya Kati kati ya Iran na Israel. Rais Donald Trump aliyekatisha ushiriki wake katika mkutano huo ameshawasili nchini Marekani.
Soma zaidi: Trump aondoka mkutano wa G7 baada ya kutoa onyo kwa Iran
Kabla ya kuondoka Canada, Trump aliungana na viongozi wengine kutoa taarifa ya pamoja inayosisitiza kuwa Iran haiwezi kuwa na silaha za nyuklia. Trump khata hivyo ameongeza kuwa anataka kuona mwisho wa kweli wa mzozo kati ya Iran na Israel na si tu kusimamisha mapigano.Katika mkutano huo Trump aliionya Iran kwamba inapaswa kuusitisha mpango wake wa Nuklia kama haijachelewa.