#HABARI: Mfamasia Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe, Halima Osman, amesema katika kuadhimisha wiki ya Famasia, wafamasia wanajukumu kubwa la kuhakikisha mgonjwa hapati usugu wa vimelea dhidi ya dawa (UVIDA).
Halima amebainisha hayo wakati alipokuwa akizungumza hali ya utoaji huduma za Famasia katika hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili Mirembe, katika kuadhimisha wiki ya Famasia yenye kauli mbiu ” Famasia kiini cha afya bora kwa wote, ubunifu, uwekezaji na afya jumuishi kwa wote chini ya uongozi wa mabadiliko” ambayo imeaanza tarehe 10 Juni hadi 16 mwaka huu.
#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania.
#Follow @radioonetanzania